Tshisekedi na Kamerhe wabatilisha uamuzi

0
1636

Viongozi wawili wa vyama vya upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo wamejitoa katika makubaliano ya kumuunga mkono mgombea mmoja wa upinzani, makubaliano yaliyofikiwa mjini Geneva, – Uswisi Jumapili iliyopita.

Felix Tshisekedi kutoka Chama Cha UDPS na Vital Kamarhe kutoka UNC walikuwa ni miongoni mwa viongozi wa upinzani waliotia saini makubaliano ya kumuunga mkono Martin Fayulu kuwa mgombea wa pamoja wa upinzani katika uchaguzi wa urais utakaofanyika Disemba 23 mwaka huu katika Jamhuri hiyo ya Kidemokrasi ya Kongo.

Wafuasi wa upinzani katika Jamhuri hiyo wameandamana katika mitaa mbalimbali ya mji mkuu wa Kinshasa kupiga hatua ya viongzoi hao wawili kujiondoa kwenye makubaliano hayo.

Awali wafuasi hao waliamini kuwa makubaliano hayo ya kumuunga mkono mgombea mmoja wa upinzani, yangeweza kuusaidia upinzani chini ya mgombea wao Fayulu kuchuana vikali na Emmanuel Ramazani Shadary, mgombea anayeungwa mkono na Rais Joseph Kabila.

Taarifa iliyotolewa na Chama Cha UDPS imesema kuwa Tshisekedi ameondoa saini yake kwenye makubaliano ya Geneva kufuatia shinikizo la wanachama wa chama hicho, uamuzi uliotangazwa na Kamerhe baada ya saa chache.