Trump na Kim kukutana tena

0
1907

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo amesema Rais Donald Trump wa Marekani na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un watakutana kwa mara ya pili hivi karibuni.

Marekani inataka muendelezo wa mazungumzo kuhusu kusitisha matumizi ya silaha za nyuklia.

Kim amemwambia Pompeo kuwa mazungumzo yake na Trump yatafanyika hivi karibuni na yupo tayari kusikiliza makubaliano watakayoyafikia.

Mara ya kwanza Kim alikutana na Trump mwezi June  mwaka huu ambapo walizungumzia kusitisha matumizi ya silaha za kinyuklia.

Pompeo yupo barani Asia ambapo amefanya ziara ya kikazi ya siku tatu katika nchi ya Japan na Korea Kaskazini ambapo hii leo pia atafanya mazungumzo na viongozi wa juu wa China.