Tetemeko la ardhi laikumba Hokkaido

0
2323

Tetemeko kubwa la ardhi limekikumba Kisiwa cha Hokkaido kilichopo Kaskazini mwa Japan na kuharibu makazi ya watu.

Vyombo vya habari katika kisiwa hicho vimeripoti kuwa watu wanane wamekufa na wengine arobaini hawajulikani walipo kutokana na tetemeko hilo.

Tetemeko hilo lenye ukubwa wa 6.7 kwenye kipimo cha mateteko, limesababisha kukatika kwa umeme kwenye nyumba milioni tatu baada ya kituo kikubwa cha kusambaza umeme kuharibiwa.

Tetemeko hilo la ardhi limetokea katika kisiwa hicho cha Hokkaido, siku chache baada ya kimbunga kikali cha Jebi kuyakumba maeneo mbalimbali ya Japan na kusababisha vifo vya watu kumi na kuharibu majengo kadhaa.