Serikali ya Ufaransa yaonya waandamanaji

0
865

Serikali ya Ufaransa imetangaza sheria kali dhidi ya waandamanaji  ikiwemo kupiga marufuku maandamano yasiyo halali na kuweka vikwazo kwa waandamanaji .

Waziri Mkuu wa Ufaransa, Edouard Philippe amesema hatua hiyoni katika kukabiliana na maandamano yasiyo na vibali kutoka Serikalini.

Serikali ya Ufaransa pia ametangaza mpango wa kuwapiga marufuku wanaosababisha fujo kushiriki katika maandamano.

Hatua hiyo inakuja baada ya maandamano yajulikanayo ”vizibao vya njano” ambayo yamedumu kwa wiki nane sasa na kusababisha ghasia na majibizano kati ya polisi na waandamanaji kwenye mji mkuu wa Paris pamoja na miji mingine ya Ufaransa.

Philippe amesema askari 80,000 watatawanywa nchi nzima katika maandamano yaliyopangwa kufanyika jumamosi ijayo.