Rais Xi Jinping afungua mkutano wa FOCAC

0
2227

Rais Xi Jinping wa China amefungua mkutano wa siku mbili wa Wakuu wa nchi na serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC).

Akifungua mkutano huo Rais Xi Jinping amesema kuwa China itatoa Dola Bilioni 60 za Kimarekani kwenye mpango wake wa miaka mitatu ya ushirikiano na Afrika katika shughuli za maendeleo.

Rais Xi Jinping ameahidi kuwa China itatoa ushirikiano ili kuhakikisha kwamba amani ya kudumu inapatikana Barani Afrika, hatua ambayo ni muhimu kwa ustawi wa nchi za Afrika.

Maeneo mengine ambayo Rais huyo wa China ameahidi kuwa nchi yake italisaidia Bara la Afrika ni ujenzi wa miundombinu, ushirikiano katika sekta ya biashara na huduma za afya.

Kadhalika Rais Xi Jinping amesema kuwa China itatoa nafasi za mafunzo ya kilimo bora na mafunzo ya ufundi kwa watalaam kutoka nchi za Afrika ili kuchangia katika

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye anamuwakilisha Rais John Magufuli katika mkutano huo alipata nafasi ya kusalimiana na Rais Xi Jinping baada ya ufunguzi wa mkutano huo.