Rais wa Sudan kuhutubia raia wake

0
919

Rais Omar Al Bashir wa Sudan muda wowote kuanzia sasa anatarajiwa kuhutubia mkutano wa hadhara mjini Khartoum, akijaribu kuwatulinza waandamanaji ambao wamekuwa wakiandamana kupinga Serikali yake.

Watu hao wamekuwa wakimshinikiza kiongozi huyo kuachia madaraka kwa madai ya kuchoshwa na sera zake na kufanya maisha yao kuendelea kuwa magumu.

Bashir amekataa mpango wa kuachia madaraka na kusema kuwa mdororo wa uchumi nchini humo kwa kiasi kikubwa na vikwazo vya kiuchumi ambavyo nchi hiyo kwa muda mrefu imekuwa ikiwekewa na jumuiya ya kimataifa.

Maandamano ya kupinga serikali yalianza nchini Sudan, mara baada ya bei ya mkate kuongezeka na bidhaa zingine zinazotokana na mafuta ya magari.

 Hata hivyo maandamano ya kudai punguzo la bei ya mkate walibadilika na kuanza kumshinikiza Bashir kuondoka madarakani.