Rais wa Nigeria ajihakikishia kushinda awamu ya pili ya uchaguzi

0
1067

Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria amesema ana uhakika wa kushinda muhula wa pili, katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 16 mwezi Februari mwaka huu.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 76 amesema hayo katika  kampeni zake za  kuelekea uchaguzi mkuu nchini  humo ambapo ujumbe wake mkubwa katika kampeni hizo ni kuendeleza vita dhidi ya ufisadi.

Hivi karibuni Rais huyo aliwaambia wafuasi wake jijini Abuja, kuwa kwa muda wa miaka minne ambayo amekuwa madarakani, ametekeleza ahadi ya kuimarisha usalama lakini pia kupambana na rushwa.

Wagombea 78 kutoka vyama 91, wanawania nafasi ya urais nchini Nigeria ambapo ushindani mkubwa katika uchaguzi huo  unatajwa kuwa ni  kati ya Buhari na mgombea wa chama kikuu cha upinzani Pdp na aliyekuwa Makamu wa rais Atiku Abubakar.