Rais Uturuki kufuatilia kupotea mwandishi wa Saudi Arabia

0
1892

Serikali ya Uturuki imesema inachukulia suala la kupotea kwa mwandishi wa habari wa Saudi Arabia, Jamal Khashoggi kama kesi ya mauaji na Rais wa  nchi hiyo Reccep Tayyip Erdogan ametangaza kuifuatilia kesi hiyo.

Umoja wa Mataifa umetaka wachunguzi wa kujitegemea kufuatilia kupotea kwa mwandishi huyo siku ya Jumanne iliyopita.

Mfalme wa Saudi Arabia amesema Uturuki inaweza ikachukua hatua ya kumtafuta mwandishi huyo katika ubalozi mdogo wa Saudi Arabia huko Istanbul kwani hawana chochote cha kuficha.

Khashoggi amekuwa akiandikia magazeti tofauti ikiwemo gazeti la Washington Post.

Rafiki wa kike wa Khashoggi amesema Khashoggi aliingia katika ubalozi mdogo wa Saudi Arabia mjini Istanbul na amekuwa akiandika habari za kuikosoa serikali ya Saudi Arabia.