Raia wa Madagascar wapiga kura

0
1329

Raia wa Madagascar wanapiga kura katika duru ya pili ya uchaguzi, kuchagua viongozi mbalimbali akiwemo Rais atakayeliongoza taifa hilo kwa kipindi kingine.

Waliowahi kuwa marais wa nchi hiyo Andry Rajoelina na Marc Ravalomanana ni miongoni mwa wagombea wa kiti cha urais nchini Madagascar.

Hii ni mara ya pili kwa wanasiasa hao wawili kuchuana katika kinyang’anyiro cha uchaguzi wa rais nchini humo.

Mara ya kwanza walichuana mwaka 2009, ambapo Ravalomanana alishindwa katika kinyang’anyiro cha urais na kulazimika kuachia madaraka.