Pompeo afanya ziara Pakistan

0
2305

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, -Mike Pompeo amefanya ziara ya siku moja nchini Pakistan, ziara yenye lengo la kuimarisha uhusiano wa nchi hizo mbili.

Katika ziara hiyo Pompeo alitarajiwa kukutana na viongozi wa Pakistan akiwemo Waziri Mkuu Imran Khan ambaye ameingia madarakani hivi karibuni.

Ziara ya Pompeo nchini Pakistan imekuja siku chache baada ya serikali ya Marekani kusitisha msaada wa kijeshi wa zaidi ya Dola Bilioni moja za Kimarekani kwa Pakistan.

Hivi karibuni Marekani ilionesha nia ya kuimarisha uhusiano wake na Pakistan ambao umeendelea kuzorota huku Marekani ikiistutumu Pakistan kwa kushindwa kukabiliana na makundi mbalimbali ya kigaidi ambayo yanafanya shughuli zake nchini humo.