Pacha watano wazaliwa Afrika Kusini

0
2293

Pacha watano wamezaliwa karibu na mji wa Johannesburg nchini Afrika Kusini.

Watoto hao wamezaliwa katika wiki ya 30 ikiwa ni mapema kwa wiki 10.

Habari kutoka nchini Afrika Kusini zinasema hao ni pacha wa tano kuzaliwa nchini humo tangu mwaka 1960.

Kwa mujibu wa Dkt. Moeng Pitsoe watoto hao wamezaliwa wakiwa na zaidi ya kilo moja kila mmoja hali inayoashiria uwezekano mkubwa wa watoto hao kuendelea vizuri.

Watoto hao waliopewa majina ya Siyanda, Sibahle, Simesihle, Silindile na Sindisiwe wataruhusiwa kuondoka hospitali baada ya kufikisha uzito wa kilo mbili kila mtoto.