Mwandishi wa habari Bulgaria auawa

0
1898

Mwandishi wa habari za kiuchunguzi wa runinga nchini Bulgaria Victoria Marinova amebakwa na kisha kuuawa.

Mwili wa mwandishi huyo mwenye umri wa miaka 30 ulikutwa katika bustani moja ya mapumziko huko Ruse ambapo simu yake, funguo za gari na nguo zake hazijaonekana.