Mnangagwa aapishwa

0
2521

Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe anayeungwa mkono na jeshi la nchi hiyo ameapishwa kuongoza Taifa hilo baada ya kushinda uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Julai mwaka huu.

Rais Mnangagwa ameapishwa na Mwanasheria Mkuu wa nchi hiyo Luke Malaba katika sherehe zilizohudhuriwa na idadi kubwa ya raia wa Zimbabwe katika uwanja wa Taifa mjini Harare.

Viongozi kutoka mataifa mbalimbali wamehudhuria sherehe hizo ambapo kwa Tanzania, Rais John Magufuli amewakilishwa na Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt Jakaya Kikwete.

Rais Mnangagwa anakabiliwa na jukumu kubwa la kuijenga upya Zimbabwe inayokabiliwa na matatizo ya kiuchumi pamoja na kuliunganisha taifa hilo.