Mlipuko wa bomu waua watu 21 nchini Colombia

0
1169

Watu 21 wamekufa na wengine 68 wamejeruhiwa kutokana na mlipuko wa bomu lilitegwa ndani ya gari nje ya chuo cha polisi nchini Colombia.

Polisi nchini humo wamesema bomu hilo lilitegwa katika gari hilo lililengwa kwa polisi waliopo katika chuo hicho cha polisi kilichopo mjini Bogota lakini raia wengi waliopo nje ndio waliouwawa pamoja na washambuliaji.

Serikali ya nchi hiyo imetangaza siku tatu za maombolezo  huku waziri wa ulinzi wa nchi hiyo akisema tukio hilo ni la kigaidi.

Ulinzi mkali umeimarishwa katika maeneo hayo ya chuo ambapo pia rais wa nchi hiyo Ivan Duque ameamrisha kuimarisha mipaka yote ya Colombia , ndani na nje ya mji.