Miili ya waliouawa yarudishwa Namibia

0
2295

Serikali ya Ujerumani imerudisha mabaki ya miili ya watu wa kabila la Horero kutoka nchini Namibia waliouwa na wakoloni wa Kijerumani katika harakati za kugombea haki nchini mwao wakati wa utawala wa kikoloni.

Wanaharakati nchini Namibia wamekuwa wakiitaka Ujerumani kuliomba kabila hilo radhi na kurejesha miili ya watu wao ambayo ilichukuliwa baada ya kuuawa kikatili na wengine kunyongwa katika ardhi ya mababu zao.

Takribani watu Elfu 75 kutoka kabila la Herero na kabila lingine nchini Namibia waliuawa na Wajerumani zaidi ya miaka 100 iliyopita baada ya majeshi ya Ujerumani kuivamia nchi hiyo ikitafuta makoloni Barani Afrika.