Meli za uvuvi za Uingereza na Ufaransa zagongana

0
2458

Meli moja ya uvuvi ya nchini Uingereza imegongana na meli nyingine ya uvuvi kutoka nchini Ufaransa huku wavuvi waliokuwa ndani ya vyombo hivyo vya majini wakitupiana maneno makali na kukaribia kupigana.

Wavuvi hao wamekuwa wakigombea eneo la kuvulia samaki ambalo wavuvi kutoka nchini Ufaransa wanaona kama wenzao kutoka Uingereza wamevamia eneo la nchi yao la bahari na hivyo kuwafanya wakose samaki.

Wavuvi wa Ufaransa wanakasirika kuwa wenzao Waingereza wamekuwa na tabia ya kuiba samaki wao kwa kuvua na kurejea makwao kwa amani huku nchini mwao wakipewa sheria kali kuhusiana na eneo hilo la baharini.

Hata hivyo wavuvi kutoka nchini Uingereza wanasema eneo hilo ni huru na wako radhi kuvua bila kufungwa na sheria yoyote.