May akutana na viongozi wa EU

0
1347

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amekutana na baadhi ya viongozi wa nchi za Umoja wa Ulaya – EU kwa mazungumzo rasmi kuisaidia Uingereza kutoka katika Umoja huo.

May amekutana na Waziri Mkuu wa Holland Mark Rutte na Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel baada ya kuahirisha kura ya kujitoa katika Umoja huo iliyokuwa ifanyike hii leo.

May amekuwa akipata shinikizo kutoka kwa wabunge wa bunge la Ulaya  kuhusu hatua yake ya kujitoa katika Umoja huo huku baadhi wakionyesha wazi kuwa watampinga wakati wa kura hiyo ya maoni.