Mawaziri wa DRC na Uganda wakutana

0
1684

Mawaziri wa afya kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) na Uganda wamekutana  kwa dharura kwa lengo la  kujadili namna ya kukabiliana na ugonjwa wa Ebola ambao tayari umesababisha vifo katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Wakati wa mazungumzo yao yanayofanyika katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Mawaziri hao pamoja na mambo mengine wanajadili namna ya kukabiliana na mlipuko mpya wa ugonjwa huo.

Tayari serikali ya Uganda imechukua hatua kwa kuanza kuwapatia chanjo wahudumu wa afya walioko mpakani mwa nchi hiyo na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Uganda imeamua kuwapatia chanjo wahudumu wake wa afya baada ya Umoja wa Mataifa kusema kuwa ugonjwa huo unaweza kusambaa hadi katika nchi zinazopakana na Jamhuri hiyo ya Kidemokrasi ya Kongo.

Hadi sasa, watu mia mbili na sitini na nane wamekufa baada ya kuugua Ebola  katika Jamhuri hiyo.