Matokeo ya uchaguzi DRC kuchelewa

0
1057

Tume ya uchaguzi katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo –DRC imesema matokeo ya uchaguzi mkuu uliomalizika nchini humo, huenda yakachelewa kutangazwa kwa vile, imeshindwa kupata matokeo ya uchaguzi kwa wakati.

Tume hiyo ya uchaguzi ya DRC imesema changamoto mbalimbali zimesababisha Tume hiyo kushindwa kupata kwa wakati matokeo ya uchaguzi huo wa Rais na wabunge kutoka katika baadhi ya vituo vya kupigia kura.

Zoezi la kupiga kura huko DRC Jumapili iliyopita pia halikufanyika katika baadhi ya maeneo kwa sababu za kiusalama na maeneo hayo kukabiliwa na ugonjwa wa Ebola.