Matokeo ya uchaguzi Drc Congo bado kutangazwa

0
1176

Upande wa upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo -Drc-umekuwa ukihoji ni kwa nini matokeo ya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo yanaendelea kuchelewa kutangazwa.

Matokeo ya uchaguzi katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo yalikuwa yatangazwa Decemba 6, lakini tume ya uchaguzi ya nchi hiyo imesema huenda matokeo hayo yakatangazwa wiki ijayo.

Hadi sasa nusu ya kura zote zilizopigwa wakati wa uchaguzi mkuu wa nchi hiyo tayari zimehesabiwa.

Upande wa upinzani huko Drc- una wasiwasi kuwa serikali ya nchi hiyo inapanga udanganyifu wa matokeo ya uchaguzi ndio maana matokeo hayo yamekuwa yakichelewa kutangazwa.

serikali ya Drc imekanusha tuhuma hizo za upinzani na kusema kuwa nchi hiyo ni kubwa na baadhi ya maeneo yako pembezoni, hiyo zoezi la kukusanya matokeo halikuwa rahisi.

hata hivyo katika baadhi ya maeneo wapinzani wameshindwa kuonyesha uvumilivu na kushiriki katika maandamano ya kupinga kuchelewa kwa matokeo ya uchaguzi wa rais, hali iliyosababisha vyombo vya usalama kutumia nguvu kutawanya maandamano hayo.