Marekani yashinikizwa kufanya uchunguzi kuhusu kashoggi

0
1927

Baadhi ya wabunge wa bunge la Seneti la nchini Marekani wameanza kuihamasisha serikali ya nchi yao kufanya uchunguzi kuhusiana na tukio la kupotea kwa mwandishi wa habari raia wa Saudi Arabia katika ubalozi wa nchi hiyo.

Wabunge hao wanataka serikali ya Marekani kutuma maafisa usalama kuchunguza mahali alipo mwandishi wa habari Jamal Kashoggi ambaye alipotea katika mazingira ya kutatanisha mara baada ya kuingia katika ubalozi wa nchi yake mjini Istanbul, -Uturuki.

Wabunge hao wametaka uchunguzi huo kufanyika baada ya gazeti la The Post la nchini Marekani kuandika kuwa serikali ya Saudi Arabia iliamuru kuwa mwandishi huyo wa habari akamatwe na kupelekwa mjini Riyadh.

Awali serikali ya Uturuki ilitangaza kuwa mwandishi huyo ameuawa ndani ya ubalozi wa Saudi Arabia, kwani tangu alipoingia kwenye ubalozi huo hajaonekana hadi  hii  leo.