Marekani yasema haioni sababu ya kutoiuzia silaha Saudi Arabia

0
2375

Rais Donald Trump wa Marekani amesema kuwa haoni sababu ya kusimamisha mauzo ya silaha kwa Saudi Arabia kwa sababu ya kutoweka kwa mwandishi wa habari wa Saudi Arabia Jamali Khashoggi.

Trump amesema kuwa Marekani inaweza kusaidia katika uchunguzi ili kubaini kilichomfika Khashoggi ambaye ni mkosoaji maarufu wa sera za Saudi Arabia.

Kashoggi alionekana mara ya mwisho akiingia katika ubalozi mdogo wa Saudi Arabia mjini Istanbul nchini Uturuki oktoba pili mwaka huu.

Vyanzo vya habari nchini Uturuki vinasema kuwa vinaamini Khashoggi aliuawa ndani ya jengo la ubalozi huo na baadaye mwili wake kuondolewa madai ambayo Saudi Arabia inayakanusha na kusema kuwa hayana msingi.