Marekani kupunguza idadi ya wahamiaji

0
2097

Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani, – Mike Pompeo amesema kuwa nchi hiyo ina mpango wa kupunguza idadi ya wahamiaji wanaoruhusiwa kuingia nchini humo ifikapo mwaka 2019.

Pompeo amesema kuwa idadi hiyo itapunguzwa kutoka wahamiaji elfu 45 kwa mwaka huu wa 2018 hadi kufikia elfu 30 mwaka 2019.

Kwa mujibu wa waziri huyo wa Mambo ya Nje wa Marekani, idadi ya wahamiaji wanaoingia nchini humo inapunguzwa ili kutekeleza sheria mpya ya uhamiaji iliyoanza kutumika.