Wizara ya Ulinzi ya Marekani imeridhia majeshi ya nchi hiyo yaliyokuwa nchini Syria kupambana na wapiganaji wa kikundi cha IS waliokuwa wakitishia usalama nchini humo kurejea nyumbani, baada ya kazi ya kuwatokomeza wapiganaji hao kumalizika.
Wakati majeshi ya Marekani yakianza kurejea nyumbani, majeshi ya serikali ya Uturuki yameanza kuelekea nchini Syria kupambana na waasi.