Maandalizi ya sikukuu za Krismas yaendelea

0
1227

Maandalizi ya sherehe za Krismas yanaendelea mjini Bethlehem, eneo ambako inasadikiwa alizaliwa Yesu Kristo.

Habari kutoka mjini Bethlehem zinasema ibada ya Krismas mwaka huu itafanyika nje ya Kanisa na Netevity ambamo Yesu alizaliwa ili kutoa fursa kwa wakristo kutoka Mamlaka ya Palestina, kushiriki kwa wazi misa hiyo.

Maelfu ya watu kutoka katika maeneo mbalimbali duniani wameanza kuwasili mjini Bethlehem kwa ajili ya sherehe za Krismas.

Desemba 25 kila mwaka waumini wa dini ya Kikristo huadhimisha kuzaliwa kwa mwokozi wao takriban miaka elfu mbili iliyopita.