Korea Kaskazini na Korea Kusini zafungua ofisi ya ushirika

0
2398

Korea Kaskazini na Korea Kusini imefungua ofisi ya Ushirika ambayo itawaruhusu kuwasiliana mara kwa mara ikiwa ni mara ya kwanza tangu vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Ofisi hiyo ambayo ipo upande wa Kaskazini mwa mpaka wa nchi hizo itachukua wafanyakazi 20 kutoka kila upande.

Waziri wa Muungano huo Cho Myoung-Gyon amesema pande hizo mbili za KOREA zitaweza kujadiliana mambo mbali mbali wakati wote.

Rais wa Korea Kusini Moon Jae-In na Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un watakutana wiki ijayo katika kilelele cha mkutano wa tatu.

Tangu Rais Donald Trump afanye mazungumzo na Kiongozi wa Korea Kaskazini mwezi June mwaka huu Korea imekubali kuacha matumizi ya nyuklia ambapo pia Kiongozi huyo wa Korea Kaskazini amemuomba Rais Trump kukutana kwa mara ya pili.