Kofi Annan afariki dunia

0
3024

Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan amefariki dunia.

Habari zinasema kuwa Annan amefariki dunia katika hospitali moja nchini Switzerland alipokua akipatiwa matibabu baada ya kuugua gafla.

Amefariki akiwa na umri wa miaka 80.

Annan alikua ni Mwafrika mweusi wa kwanza kutumikia wadhifa huo wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na alitumikia nafasi hiyo kwa vipindi viwili kati ya mwaka 1997 na 2006.