Kimbunga Michael chasababisha uharibifu Florida

0
1942

Kimbunga Michael tayari kimelipiga jimbo la Florida nchini Marekani na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali na miundombinu ambao haujawahi kutokea katika jimbo hilo katika kipindi cha miaka kumi iliyopita.

Kimbunga hicho ambacho hivi sasa kinaelekea katika jimbo la jirani la Georgia huku kikiwa kimesababisha baadhi ya mapaa  katika jimbo la Florida kung’olewa na kutupwa mbali.

Kimbunga Michael pia kimesababisha mafuriko na kung’oa miti mikubwa  ambayo mingine imeangukia barabarani na kutatiza mawasiliano ya barabara katika jimbo hilo.