Kimbunga Jebi chaikumba Japan

0
2305

Watu kumi wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya kimbunga Jebi kuyakumba maeneo mbalimbali nchini Japan.

Taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Japan imesema kuwa kimbunga hicho ni kibaya kuwahi kutokea nchini humo ndani ya kipindi cha miaka 25.

Kimbunga hicho kimesababisha uharibifu mkubwa wa majengo na miundombinu hasa katika miji iliyo Magharibi mwa nchi hiyo ambayo ni pamoja na Kyoto na Osaka.

Habari zaidi kutoka nchini Japan zinasema kuwa njia za usafiri wa anga, treni na vivuko zilisitishwa kwa muda kuhofia madhara ya kimbunga hicho aina ya Jebi.

Hadi sasa zaidi ya watu Mia Tatu wamejeruhiwa kufuatia kimbunga hicho .