Kifaa cha kuwasaidia waliopooza chagunduliwa

0
2286

Wanasayansi nchini Uswisi wamegundua kifaa maalum kinachotumia umeme ambacho kinatarajiwa kuwasaidia watu waliopooza viungo mbalimbali vya mwili hasa uti wa mgongo kupona na kurejea katika hali ya kawaida.

Kifaa hicho kina uwezo wa kusisimua misuli ya mgongo na kuunganisha ufahamu katika ubongo wa binadamu ili hatimaye kurejesha mawasiliano yaliyokatika kati ya ubongo na uti wa mgongo.

Hata hivyo zoezi hilo sio rahisi, kwa kuwa mgonjwa anapaswa kupitia katika mazoezi mengi, wakati mwingine kuhisi maumivu makali, lakini mwisho ni kumsaidia kurejea katika maisha yake ya kawaida.