Kesi ya mfanyabiashara ya dawa za kulevya yaanza kusikilizwa Marekani

0
1269

Kesi ya kuhusika na biashara haramu ya dawa za kulevya na mauaji inayomkabili mfanyabiashara maarufu wa dawa hizo, pamoja na kiongozi wa genge la uhalifu El chapo au Gus Man, imeanza kusikilizwa nchini Marekani.

El chapo ambaye ni raia wa Mexico alipelekwa nchini Marekani ili kukabiliana na kesi yake, baada ya kuonekana kuwa ni mahabusu hatari, kwani mara kadhaa ametoroka gerezani alikokuwa akishikiliwa nchini Mexico.

Gus Man, mara kadhaa kwa msaada wa wafuasi wake amewatoroka polisi waliokuwa wakimtafuta au kutoroka gerezani hata katika magereza yenye ulinzi mkali.

Mara ya mwisho El chapo alitoroka kupitia handaki lililokuwa kwenye mahabusu hadi umbali mrefu nje ya gereza na kisha kuchukuliwa na helikopta.