Keita aapishwa kuiongoza Mali

0
2331

Rais mpya wa Mali Ibrahim Boubcar Keita ameapishwa baada ya kushinda uchaguzi mkuu uliofanyika Agosti 12 mwaka huu.

Sherehe za kuapishwa kwa Keita zimefanyika katika viwanja vya Kouluba chini ya ulinzi mkali.

Agosti 20 mwaka huu mahakama ya kikatiba nchini Mali ilimthibitisha Keita kuwa mshindi wa kiti cha Urais na kutupilia mbali mashitaka yaliyofunguliwa na mpinzani wake Soumaila Sisse’s kwa madai kuwa uchaguzi huo uligubikwa na vitendo vya rushwa.