Kansela Angela Merkel ziarani Nigeria

0
2723

Kansela Angela Merkel wa Ujerumani ameanza ziara yake nchini Nigeria ikiwa ni ziara ya mwisho kwa nchi za Afrika Magharibi.

Kabla ya kuanza ziara yake nchini Nigeria, Kansela Merkel alikua na ziara katika nchi za Senegal na Ghana ambapo pamoja na mambo mengine alikutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa nchi hizo.

Lengo la ziara hiyo ya Kansela wa Ujerumani nchini Nigeria ni kukuza uhusiano wa kiuchumi baina ya nchi yake na nchi hiyo pamoja na kuangalia namna ya kupunguza suala la wahamiaji wanaoingia Barani Ulaya.

Wakati wa mazungumzo yake na Rais Muhammadu Buhari wa nchi hiyo, Kansela Angela Merkel anatarajiwa kugusia masuala ya ulinzi pamoja na uchaguzi mkuu ujao wa Nigeria.