Kamata kamata yaendelea Ethiopia

0
1595

Ethiopia imewakamata zaidi ya watu sitini kwa tuhuma za ufisadi na ukiukaji wa haki za binadamu, wakiwemo maafisa wa upelelezi, askari na wafanyabiashara.

Watu hao wamekamatwa kufuatia amri iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Ethiopia, – Abiy Ahmed na wamekamatwa baada ya kufanyika kwa uchunguzi uliodumu kwa miezi kadhaa kuhusu makosa mbalimbali yaliyotokea chini ya utawala wa watangulizi wake.

Ofisi ya mwendesha mashtaka nchini Ethiopia imesema kuwa baadhi ya watu waliokamatwa wanashutumiwa kuwatesa wafungwa huku wakiwalazimisha kukiri makosa yao, kuwadhalilisha watu, kuwatesa watuhumiwa wa uhalifu kwa kutumia nyaya za umeme na hata kuwaua.

Tangu alipoingia madarakani mwezi Aprili mwaka huu, Abiy amewaachilia huru maelfu ya wafungwa na kufanya mageuzi mengine makubwa ya kisiasa nchini Ethiopia.