Jukwaa la Utalii, Uwekezaji na Biashara lafanyika nchini Ghana

0
202

Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria, Wenye Uwakilishi Sambamba nchini Ghana, umefanya Kongamano la Utalii, Uwekezaji na Biashara (Tanzania-Ghana Tourism, Investment and Trade Forum (TN-TITF), kwa lengo la kutangaza utalii na kuvutia wawekezaji kutoka nchini Ghana kuja kuwekeza hapa nchini.

Jukwaa hilo liimefunguliwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula, ambapo pia limehudhuriwa na wadau wa sekta mbalimbali ikiwemo Jumuiya za Wafanyabiashara, Wenyeviwanda, Kilimo na Madini za Ghana, Makampuni ya Utalii, Wafanyabiashara na Wawekezamitaji.

Aidha, Taasisi za Tanzania, hususani TTB, TIC, ZIPA, EPZA, TanTRADE, Jumuiya za Wafanyabiashara, Wenyeviwanda, Kilimo na Madini za Tanzania Bara na Zanzibar, zilishiriki na kuelezea kwa undani fursa, miundo, majukumu na nafasi zake katika kukuza Biashara, Utalii na Uwekezaji nchini Tanzania.

Balozi wa Tanzania nchini Nigeria anbaye pia anawakilisha nchi ya Ghana Dkt. Benson Bana, ameeleza kuwa Jukwaa hilo linakusudia kuleta taasisi, jumuiya za wafanyabiashara, wawekezaji wa Tanzania na Ghana kuona namna ya kushirikiana na kukuza mahusiano ya uwili baina ya nchi hizo, ambazo uhusiano wake ulianza tangu kipindi cha waasisi wa mataifa hayo.

Kwa Upande wake Balozi Mstaafu wa Ghana nchini Ufaransa, Genevieve Delali Tsegah, amepongeza hatua hiyo na kusema kuwa itakwenda kufungua milango ya utalii na uwekezaji nchini Tanzania kutokana na kazi kubwa inayofanywa na viongozi wake