Jaribio la mapinduzi Gabon ladhibitiwa

0
1178

Serikali ya Gabon imesema imerejesha hali ya utulivu nchini humo, baada ya kikundi cha askari waasi kufanya jaribio la mapinduzi, katika kipindi hiki ambapo Rais wa nchi hiyo Ali Bongo yuko nchini Morocco kwa matibabu.

Msemaji wa serikali ya Gabon amesema watu wanne wanaotuhumiwa kufanya jaribio hilo wamekamatwa.

Mapema leo baadhi ya askari walidai kufanya jaribio la mapinduzi nchini Gabon kwa lengo la kurejesha demokrasia nchini humo ambapo magari yenye silaha yalionekana katika mitaa ya mji mkuu wa Gabon, Libreville.