Iran yapingana na Marekani kuhusu vikwazo

0
2322

Marekani imesema kuwa mahakama ya kimataifa ya makosa ya uhalifu wa kivita haina uwezo wa kusikiliza kesi ya madai ya kuzuia vikwazo ambavyo nchi hiyo imeiwekea Iran.

Iran inataka kuwasilisha madai yake kwenye mahakama hiyo ili kuizuia Marekani kuiwekea vikwazo vipya vya kiuchumi.

Vikwazo hivyo vipya viliwekwa na Marekani dhidi ya Iran wiki mbili zilizopita baada ya Rais Donald Trump wa nchi hiyo kutupilia mbali makubaliano ya mpango wa nyuklia yaliyofikiwa na Jumuiya ya Kimataifa mwaka 2015.