Houthi wasema wako tayari kwa mazungumzo

0
1482

Wawakilishi wa Wanamgambo wa Houthi wa nchini Yemen wamewasili nchini Sweden kwa ajili ya mazungumzo ya amani ya nchi yao.

Wawakilishi hao wamesema kuwa wako tayari kujadiliana kuhusu masuala kadhaa ya nchi yao ikiwa ni pamoja na kutafuta njia zitakazowezesha misaada ya kibinadamu kuwafikiwa walengwa wakati Yemen ikiwa katika vita.

Wanamgambo hao  wa Houthi wanashikilia sehemu kubwa ya nchi ya Yemen, wakati serikali iliyoko madarakani ikiendesha shughuli zake uhamishoni.

 Majeshi ya Saudi Arabia yakishirikiana na majeshi ya nchi washirika yamekuwa yakiwashambulia Wanamgambo hao wa  Houthi kwa lengo la kuisaidia serikali iliyopo madarakani.