Hali ya utulivu kurejea nchini Brazil

0
1042

Serikali ya Brazil imepeleka askari wake katika mji wa Fortaleza ulikoko kaskazini mwa nchi hiyo kurejesha hali ya utulivu baada ya vitendo vya uhalifu kuongezeka kwenye mji huo katika siku za hivi karibuni.

Matukio yapatayo themanini yameripotiwa katika jimbo la Sariya katika eneo hilo, ikiwa ni pamoja na vitendo vya ujambazi, unyang’anyi wa kutumia nguvu na mashambulio dhidi ya watu kwa kutumia kemikali zenye athari kwa maisha ya binadamu.

Magenge ya wafanyabiashara haramu wa dawa za kulevya yamekuwa yakihusika na matukio hayo ya uhalifu kuanzia kwenye magereza ya nchi hiyo hadi mitaani.

Serikali mpya iliyoingia madarakani, iliahidi kuwachukulia hatua kali watu wote wanaohusika na biashara haramu ya dawa za kulevya.