Hali ya kawaida yarejea Indonesia

0
1905

Siku kadhaa baada ya tetemeko la ardhi kuikumba Indonesia watoto katika mji wa Palu wameanza kurejea shule kufanya usafi kwenye baadhi ya vyumba vya madarasa ambavyo havikupata madhara.

Mkuu wa shule moja huko Kasiludin amewataka walimu wote kuhudhuria shule hii leo na kutoa taarifa za wanafunzi walioanza kuhudhuria masomo na taarifa za wale ambao wamefariki dunia.

Tetemeko hilo la ardhi limeua watu zaidi ya 1900, wengine 2500 wamejeruhiwa na 5000 hawajulikani walipo na zoezi la kuwatafuta watu wengine linatarajiwa kusitishwa Alhamisi wiki hii.