Gbagbo azuiwa na Icc kuondoka nchini Uholanzi

0
911

Mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai Icc, iliyoko huko The Hague, Uholanzi  imemzuia rais wa zamani wa Ivory Coast,Laurent Gbagbo, kuondoka nchini humo licha ya kuachiwa huru.

ICC imemzuia Gbagbo kuondoka Uholanzi, akiwa anajiandaa kurejea nchini mwake, baada ya waendesha mashtaka katika mahakama hiyo kukata rufaa dhidi ya kesi inayomkabili ya kuhusika na makosa ya uhalifu wa kivita nchini mwake.

Gbagbo anatuhumiwa kutenda kosa hilo miaka minane iliyopita, mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa Ivory Coast uliompatia ushindi mpinzani wake mkuu Alsane Outtarra, na yeye kukataa kuondoka madarakani.

Askari waliokuwa wakimuunga mkono mwanasiasa huyo walipita nyumba kwa nyumba kuwasaka wapinzani wake na kuwaua pamoja na raia wa kigeni, hali iliyosababisha watu wapatao elfu tatu kupoteza maisha nchini Ivory Coast.

Wafuasi wa Gbagbo walionekana kushangilia, baada ya Icc kutangaza kuwa imemwachia huru mwanasiasa huyo, baada ya kukosekana ushahidi wa kumtia hatiani.

Hata hivyo baadhi ya watu ambao ndugu za walikufa wakati wa mapigano hayo ya wenyewe kwa wenyewe nchini Ivory coast walionekana kukosa amani.