Eritrea na Somalia kuimarisha uhusiano

0
1824

Rais Isaias Afwerki wa Eritrea yuko mjini Mogadishu nchini Somalia kwa ziara ya kikazi, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha uhusiano baina ya mataifa hayo mawili.

Nchi za Somalia na Eritrea zimeamua kufufua uhusiano wa kidiplomasia kwa maslahi ya raia wa mataifa hayo mawili.

Kwa miaka kumi na mitano, mataifa hayo mawili yamekuwa hayana uhusiano wa kidiplomasia.

Somalia imekuwa ikiishutumu Eritrea kwa kuwaunga mkono wanamgambo wa Al Shabaab wa nchini Somalia.

Nchi hizo mbili zilitiliana saini kuanza rasmi uhusiano wa kidiplomasia mwezi Julai mwaka huu.