China yafungua daraja refu zaidi duniani

0
2145

Rais Xi Jinping  wa China amefungua daraja refu zaidi duniani lenye urefu wa kilometa 55 linaloyaunganisha maeneo mawili ya Hong Kong na Macau.

Sherehe za ufunguzi wa daraja hilo zimepambwa na burudani mbalimbali na kuhudhuriwa na viongozi wakuu wa miji ya Hongkong na Macau.

Ujenzi wa daraja hilo lililovunja rekodi umeigharimu China Dola bilioni  Ishirini za Kimarekani na umechukia muongo mmoja kumaliza ujenzi wake.

Daraja hilo ambalo limejengwa kuhimili matetemeko makubwa ya ardhi na vimbunga, linajumuisha njia ya urefu wa kilimota 30 iliyopita kwenye mlango wa Mto Pearl na linajumuisha pia visiwa viwili vidogo vya kujengwa na binadamu.

Ufunguzi wa daraja hilo unaelezwa kuwa utapunguza muda wa safari kutoka Hong Kong hadi China kwa hadi dakika 30 badala ya saa nne, jambo ambalo China imesema kuwa itakuwa kiungo muhimu kwa ukuaji wa uchumi katika siku zijazo.