China Kuchunguza Mashtaka ya Rushwa Yanayomhusu Meng

0
1875

Serikali ya China imevunja ukimya na kusema inachunguza  mashtaka ya rushwa ambayo wanayahusisha na kupotea kwa kiongozi wa shirika la Polisi duniani Interpol, Meng Hongwei.

Mke wa Meng amesema anahisi mumewe yupo China na atakuwa kwenye hali ya hatari kwani baada ya kumkosa mumewe alipiga simu katika ofisi za Shirika hilo huko Ufaransa.

Meng hajapatikana tangu Septemba 25 alipoondoka kwenda China kwa ziara binafsi ambapo taarifa za kupotea kwake zilianza kusikika wiki  iliyopita.

Taarifa zinasema Meng aliachia nafasi ya urais wa Shirika hilo la Polisi lenye makao makuu yake nchini Ufaransa katika mji wa Lyon.