Burna Boy kinara wa Tuzo za Soundcity

0
303

Mwanamuziki wa Nigeria Burna Boy ameibuka kinara kwenye Tuzo za Muziki za Soundcity baada ya kuchukua tuzo 3 ambazo alikuwa akishindana na wakali wa muziki kama vile Davido, Wizkid, Tiwa Savage, Sho Madjozi na Diamond Platnumz

Vipengele alivyochukua ni Best Male MVP(mwanamuziki bora wa kiume), Song of the Year (wimbo bora wa mwaka) na African Artist of the Year (msanii bora wa Afrika kwa mwaka).