Buhari ajitokeza, asema atawania tena Urais

0
1424

Rais Muhamadu Buhari wa Nigeria amejitokeza hadharani na kukanusha uvumi kuwa amefariki dunia, uvumi uliokua ukienea katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwa miezi kadhaa sasa.

Buhari ambaye atakuwa anawania kuchaguliwa tena katika uchaguzi wa Urais nchini Nigeria mwezi Februari mwaka 2019, alikuwa nchini  Uingereza kwa  muda mrefu akipatiwa matibabu ya maradhi ambayo hayajawekwa wazi.

Kumekuwa na uvumi kuwa Rais  Buhari amefariki dunia na nafasi yake imechukuliwa na mtu anayefanana naye, ambaye anatoka nchini Sudan.

Buhari amesisitiza kuwa anayeiongoza  Nigeria ni yeye na kwamba hivi karibuni atakuwa anaadhimisha mwaka wake wa 76 wa kuzaliwa.