Askari mmoja afariki baada ya kulipukiwa na bomu

0
1026

Askari polisi mmoja amekufa mjini Cairo nchini Misri alipokuwa akijaribu kutegua bomu lililokuwa limetegwa karibu na kanisa moja kwenye mji huo.

Askari wengine wawili waliokuwa wakisaidia na askari polisi huyo kutegua bomu hilo wamejeruhiwa, baada ya kushindwa kuliwahi bomu hilo na kisha kulipuka.

Bomu hilo lilikuwa limetegwa siku mbili kabla ya wakristo wa madhehebu ya Coptic nchini humo kusherehekea sikukuu ya Krismas.

Mara kadhaa yametokea mashambulio katika makanisa ya kikristo nchini Misri na kusababisha maafa na hivi sasa Serikali ya nchi hiyo inaendelea kuimarisha ulinzi ili kudhibiti milipuko kama hiyo inayolenga mikusanyiko ya watu.