Amnesty International yashutumu adhabu ya kifo kwa watoto

0
1689

Ripoti iliyotolewa na Shirika la Kutetea Haki za Binadamu  la Amnesty International kuhusu adhabu ya kifo nchini Sudan Kusini imesema kuwa,  watoto ni miongoni wafungwa wanaonyongwa nchini humo.

Shirika hilo limesema kuwa watu saba  akiwamo mtoto mmoja  wamenyongwa na serikali ya Sudan katika kipindi cha kuanzia mwaka huu hadi hivi sasa,  idadi ambayo ni kubwa nchini humo tokea kuasisiwa kwake mwaka 2011.

Kwa mujibu wa Amnesty International, wafungwa wawili ambao walikuwa watoto walipohukumiwa walinyongwa mwaka 2017.

Kwa muda mrefu, Sudan Kusini imekua katika vita ya wenyewe kwa wenyewe hadi kulipofikiwa makubaliano ya amani hivi karibuni.

Makundi mbalimbali ya Wanamgambo nchini humo yalikuwa yakitumia maelfu ya watoto kama Askari, hali iliyosababisha watoto hao kukabiliwa na makosa mbalimbali.