Ajali ya ndege yaua 19 Sudan Kusini

0
2294

Watu 19 wamekufa baada ya ndege ndogo ya abiria kuanguka kwenye ziwa Yirol wakati ikijaribu kutua huko Sudan Kusini.

Watu wanne tu, wawili wakiwa watoto wamenusurika katika ajali hiyo.

Habari kutoka Sudan Kusini zinasema kuwa wakati ajali hiyo inatokea, ndege hiyo ilikua na watu 23 ambao ni wafanyakazi pamoja na abiria.

Ndege hiyo ndogo ilikua ikisafiri kutoka mji wa Juba kuelekea mji wa Yirol na chanzo cha ajali hiyo kinaelezwa kuwa ni hali mbaya ya hewa kwani kulikua na ukungu.

Rubani wa ndege hiyo alijaribu kutua katika eneo salama ikashindikana na badala yake ndege hiyo ikaanguka katika ziwa Yirol eneo ambalo ni karibu na mji wa Yirol ambapo ndege hiyo ilitakiwa itue.