Wimbo wa Mwanza wapigwa stop na BASATA

0
1940

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA ) limeufungia rasmi wimbo unaojulikana kama Mwanza ulioimbwa na msanii wa lebo ya Wasafi, -Raymond Mwakyusa maarufu kama Rayvanny na kumshirikisha mwanamuziki mwenzake Naseen Abdul maarufu kama Diamond Platinumz.

Katibu Mtendaji wa BASATA, – Geofrey Mngereza amesema kuwa wameamua kuufungia wimbo huo kutokana na ukiukaji wa maadili ya Kitanzania kwa msanii Rayvanny ambaye ametumia maneno ya udhalilishaji.

Pamoja na kuufungia wimbo huo, BASATA pia imewataka wasanii, vyombo vya habari na mtu yoyote kutoutumia, kutoucheza ama kuusambaza kwa namna yoyote ile.

BASATA imewataka msanii Rayvanny, Diamond pamoja na uongozi wa kampuni ya Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa.

Kampuni hiyo ya Wasafi imeagizwa kuuondoa wimbo huo kwenye mitandao ya kijamii mara moja kabla ya saa 12 kamili jioni Novemba 12 mwaka huu.